Jumatano, 4 Machi 2020

DAMU YA YESU KRISTO

YOHANA 1:29

TAZAMA MWANAKONDOO WA MUNGU AICHUKUAE DHAMBI YA ULIMWENGU.
   " KWAKUWA TORATI ILITOLEWA KWA MKONO WA MUSA, NEEMA NA KWELI ZILIKUJA KWA MKONO WA YESU KRISTO   -YOHANA1:17"

 Ndugu katika Kristo Yesu ni Vema kuchagua kujua Umuhimu wa Sadaka ya Mungu yaani Yesu Kristo Mwanakondoo asiye na mapungufu wala dhambi,
Katika agano la Kale zilitumika Sadaka za wanyama kuleta upatanisho kati ya Mungu na Mwanadamu.
Katika agano jipya yaani Mungu amemwachilia mwanaye wa pekee Yesu Kristo awe Sadaka( yaani kafara) Takatifu
   UFUNUO 5:9(KWA KUWA ULICHINJWA UKAMNUNULIA MUNGU KWA DAMU YAKO WATU WAKILA KABILA NA LUGHA NA JAMAA NA TAIFA)..

   1.Ni vema kuamini Kifo cha Yesu kimerejesha mahusiano kati ya Mungu na Mwanadamu wa kila ukoo,kabila na taifa
   2. Ni vema kujua na kuamini kuitumia Damu ya Yesu kujitakasa Toka maisha machafu ya dhambi.
   3.Ni vema kuamini kuwa wanaotumia Damu za wanyama wako nje ya agano la Yesu wanatenda dhambi na wanaalikwa kuitumia Damu ya Yesu Wapate Utakaso na Kibali.

 DAMU YA YESU ILIYOMWAGIKA MSALABANI KWA AJILI YA WENGI KUWAONDOLEA DHAMBI

KAMA INAVYOFAFANULIWA

 (WARUMI 5:19-kwa sababu kama kwa kuasi kwake mtu  mmoja {Adamu} watu wengi waliingizwa katika dhambi,kadhalika kwa kutii kwake mmjo{Kristo} watu wengi wameingizwa katika hali ya
 haki)
""Hivyo Haki Hupatikana katika Kristo aliyefanyika dhambi ili wengi{watu} wapate Haki kwa Njia ya Msamaha""

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni