Jumapili, 5 Machi 2023

IMANI YA KIMUNGU

(Ebrania 11:1-) Imani ya Kimungu ni kuwa na uhakika wa mambo unayoyatarajia kutoka kwa Mungu, ni bayana ya mambo yasiyoonekana. AU Imani ni kuwa na uhakika wa mambo unayoyatarajia kutoka kwa Mungu, Ni bayana ya mambo uliyoyaumba/yaliyoumbwa ulimwengu wa roho kwa neno lako au kwa neno la Mungu kabla mambo hayo hayajatokea au kudhihirika kwa macho ya kawaida. Kwa Imani twafahamu ya kuwa Ulimwengu uliumbwa kwa neno la Mungu., na Vitu vinavyoonekana havikufanywa kwa vitu vilivyo dhahiri/vinavyoonekana. HATUA ZA MSINGI KUJENGA IMANI i. Kuwa na Wazo (luka 12:17) ii. Kulitafakari/kulimeng’enya iii. Kupata uhakika kuwa wazo ni sahihi/kuwa na msimamo/ kuwa na amani ya Kristo. iv. Kulikiri kwa kinywa mbele za Mungu kwanza na kwa watu wanakuhusu. Kwa mfano, Mbunifu wa Majengo huumba/hubuni nyumba akilini mwake kabla yakuanza kuleta matofali na mawe Hutazama mwisho kwanza ndipo huanza kujenga (Isaya 46:10 nitangazaye mwisho tangu mwanzo,) Katika Imani ya Kimungu , Atoaye wazo sahihi ni Roho wa Mungu moyoni mwa mtu kupitia NENO LA KRISTO ambalo ni mbegu/wazo Baada ya kulichakata moyoni na nafsini hufuatia hatua ya kulipeleka kwa Mungu ili liumbike ulimwengu wa roho, ili kupitia nguvu ya IMANI ya mtu alivute au alikokote jambo hilo litokee katika ulimwengu wa Mwili kwa majira yake sahihi. i. Lipo linatokea papo kwa papo (Luka 4:35) ii. Lipo linatokea kwa masaa (Ebrania 11:17) iii. Lipo linalotokea kwa miezi na miaka (Isaya 7:14) Katika Imani ya kimungu kuna namna mbili za Imani :- i. Imani ya kupokea vitu vilivyokinyume na kanuni za kimwili au kijografia kama ilivyotokea kwa baadhi ya watu wa Mungu . Mfano:- .Joshua kusimamisha Jua/Dunia .Kukaushwa bahari ya shamu .Bikira kuzaa mwana .Yesu kufufuka kati ya wafu Katika Imani hii kuna nyenzo ya ziada ambayo ni Karama ya Imani kukusaidia katika kukamilika kwake. (1korinto 12:9 mwingine imani katika Roho yeye yule;) Omba karama ya Imani kama unamalengo yaliyojuu ya akili ya kibinadamu. ii. Imani ya kupokea vitu vya kawaida Kupona magonjwa, kufanikiwa kiuchumi, kupata mme/mke, kuongezwa cheo nk. Haya yote nimeyaweka katika kundi la Imani ya kawaida kwa sababu ni mwaliko wa kiujumla kwa kila aaminiye kama ilivyoandikwa “mwenye haki ataishi kwa Imani”(Ebrania10:38) KILA ALIYE NDANI YA KRISTO ANAYO IMANI. Kristo ndiye Mwanzilishi wa Imani yetu hivyo ameweka imani ndani yetu kupitia Roho wake anayetufundisha neno la Mungu kila siku. Swali:- Kama nina Imani kwanini ninamengi niliyoomba sijapokea? KWANINI SIPOKEI NILICHOOMBA KWA MUNGU i. Wazo lisilo na maslahi na Mungu , kwa mfano unatakuoa/kuolewa alafu unasema nataka mke wangu au mme awe na kazi fulani na mshahara fulani, ukikosa ulichoomba usilaumu mtu jilaumu wewe, n.k ii. Uoga , mara zote Yesu amewaonya wanafunzi akisema msiogope, uoga kwa watu wa Afrika ni mkubwa sana kiasi kwamba wanyama kama paka na bundi bado wana mamlaka mioyoni mwa watu. iii. Kuongea kinyume na ulichoumba kwa maombi . Mfano. Nchi hii kufanikiwa ni vigumu sana alafu jana usiku uliomba upate mtaji/kazi au unasema ninaumwa kaugonjwa ketu ila jana uliomba uponyaji, Utaishia kuomba bila majibu miaka yote. JIFUNZE HATUA HIZI UTAMWONA MUNGU MACHONI PIA 1. Wazo/neno la Mungu moyoni mwa mtu:- Nataka kupona ugonjwa neno msingi (Math 8:17 aliuchukua udhaifu wetu Na kuyachukua magonjwa yetu.) 2. Kutafakari neno au wazo hilo moyoni na akilini kuona Upendo na Huruma ya Mungu katika kukuponya (Luka 2:35 ili yafunuliwe mawazo ya mioyo mingi) 3. Kuomba au kuwasilisha kwa Mungu akamilishe nia yake ya kuwaponya watu (Yohana 10:10 mimi nalikuja ili wawe na uzima, kisha wawe nao tele) 4. Kubadili mtazamo usikione unachoona machoni yaani ule ugonjwa, badala yake ona kile kilichopo ulimwengu wa roho yaani uponyaji/uzima. katika hili hakusaidii mtu mwingine hata mtumishi wa Mungu ni wewe binafsi 5. Kiri kushinda wakati wote hata kama wanakucheka kuwa umechanganyikiwa kwa kusema kitu wasichokiona wenzako na adui wa Imani yako mkubwa ni yule mnayeheshimiana anaweza kuwa mtumishi pia , ukiwashinda wakatisha tamaa unaowaheshimu, basi Mungu hana kizuizi cha kudhihirisha/kuprinti kilichokuwa rohoni kuja mwilini, ndipo utasikia pongezi kwa wale wakatisha tamaa. MUNGU AKUBARIKI KATIKA TAFAKARI HII YA NENO LAKE

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni