Alhamisi, 15 Februari 2024

JIFUNZE KUTOPUUZIA MAMBO MADOGO NA KUTOCHUKULIA KAWAIDA MAKOSA MADOGO MADOGO

JIFUNZE KUTOPUUZIA MAMBO MADOGO NA KUTOCHUKULIA KAWAIDA MAKOSA MADOGO MADOGO Mfano imetokea nimelala mpaka asubuhi bila kuamka na kufanya maombi, isichukulie kawaida. Usipuuzie. Inatakiwa moyoni uumie na kujiuliza, Ni Kwanini sijaamka kuomba ?! Inamaana nimeshindwa kuwa na muda na Mungu hata kwa muda mfupi Usiku mzima ?! Yesu hakuchukulia kawaida kwa akina Petro kushindwa kuomba pamoja naye usiku ule, akawaamsha na kuwauliza, hamkuweza kukesha hata saa moja ?! HATA KAMA WATU WENGINE WATACHUKULIA KAWAIDA LAKINI WEWE USIPUUZIE WALA KUONA NI KAWAIDA, SHITUKA Imetokea Siku nzima inapita sijapata muda wa KUSOMA BIBLIA, Au nimeamka na kuendelea na majukumu yangu bila KUMSHUKURU MUNGU KWA KUNIAMSHA SALAMA. Au nimesinzia bila kusali usiku KUJIKABIDHI KWA MUNGU. Au siku nzima inapita sikupata muda wowote wa kuongea na Mungu kwa Sala na maombi. Kamwe usipuuzie au kuchukulia kawaida makosa madogo madogo ya aina hiyo, usikubali uongo ambao adui anakwambia eti ulikuwa bize hata Mungu anajua. Ukweli ni kwamba, wakati mwingine unasumbuka na mambo mengi wakati unaliacha FUNGU LILILO JEMA AMBALO HALIPOTEI, Jiulize, kwa nini hata kama uko bize kiasi gani, lazima uwe na muda wa kula, hata uwe bize kiasi gani, lazima baadaye utapumzika au utalala usingizi hata kama ni kwa kuchelewa, hata uwe bize kiasi gani, lakini asubuhi unapoamka unapata muda wa kuvaa nguo, kupiga mswaki n.k Kama pamoja na ubize wote ulionao, bado kuna mambo hautaacha kuyafanya ili uendelee kuonekana nadhifu na pia ubaki na nguvu za kuendelea kufanya kazi, Unakosaje ratiba muhimu ili roho yako iendelee kuwa na afya pia Mungu aendelee kukutetea ?! Kwa nini usitumie dakika kadhaa kabla ya kula, kulala, kuvaa nguo, kuoga n.k ukaanza kuomba au kusoma biblia kisha ukaendelea na ratiba zako ?! KINACHOKUZUIA SIO UBIZE, BALI NI KUTOONA UMUHIMU WA NENO NA MAOMBI KWENYE MAISHA YAKO. CHOCHOTE AMBACHO UNAJUA KINA UMUHIMU KWENYE MAISHA YAKO LAZIMA UTAKIPA NAFASI KWENYE RATIBA ZAKO ZA UBIZE, KADHALIKA NA YESU AKIWA NA UMUHIMU KWAKO, LAZIMA UTATAFUTA MUDA WA KUONGEA NAYE. Tabia ya kupuuzia au kuchukulia kawaida makosa madogo madogo, baada ya muda huwa inakomaa na kuwa tabia halisi. Yaani inakuwa ni tabia yako Kulala bila kusali, kuamka bila KUMSHUKURU MUNGU, Inakuwa ni tabia yako kutokusoma Neno la Mungu na kutofanya maombi. Wengine tayari wameshakuwa na tabia hata ya kutosali Jumapili au kuhudhuria vipindi vya katikati ya wiki, Mungu atusaidie sana. Inapaswa nianze kuwa na mtazamo kwamba, nisipofanya yale ninayopaswa kufanya nijihisi kama nimemkosea Mungu, natakiwa nirudi mbele za Mungu kuomba toba. Nimwambie Mungu nimekuwa mzembe naomba unisamehe. UJUE KUNA MAISHA UKIYAISHI DHAMBI INAKUWA HADITHI KWAKO UTAKUWA UNAISIKIA KWA WATU WENGINE TU Sasa Wengi hawajui Kuwa kupuuzia makosa madogo madogo Huwa inaleta mazoea Hatimaye inakomaa inakuwa Ndiyo tabia ,na ikashakua tabia ni ngumu Sana kuja kujirekebisha Sababu inakuwa imeshaota mizizi. Hata watu walioanguka kwenye dhambi, nao walianza kwa kupuuzia mambo madogo madogo, kadhalika hata Samsoni alikamatwa baada ya kuchukulia kawaida maneno ya Delila akiona kama ni utani, kumbe alikuwa ametumwa kwa lengo la kumdhoofisha ili adui wamkamate. Kama unataka kufika viwango Vya Juu Kiroho Moja kati ya Jambo ambalo unapaswa kulizingatia basi ni hili Epuka kuyapuuzia makosa madogo madogo na kuyachukulia Kawaida Kabisa Hata kama wengine wanachukulia Kawaida lakini wewe usiyachukulie Kawaida Unapogundua Kuna kosa lolote umelifanya usilipuuzie lilekebishe chapchap Unapogundua Kuna Mahali haupo sawa mfano umepunguza viwango Vya Maombi ,kusoma Neno , umepunguza Muda Wako na Mungu usipuuzie rekebisha haraka Sana kabla halijageuka Kuwa mazoea halafu Kuwa tabia Jifunze hili Kama unataka Kufika mbali Kiroho Maana mambo ya Kiroho yanahitaji NIDHAMU KUBWA SANA HAYATAKI MCHEZO MCHEZO ,HAYATAKI MASIHARA MASIHARA BARIKIWA KWA UJUMBE HUU.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni